Na Zaynab Nyamka, Globu ya Jamii.

BAADA ya kuchukua tuzo ya mchezajo bora wa Shirikisho ijulikanayo kama PFA Player of the Year akiwa tayari ameshachukua tuzo ya kila mwezi mara tatu katika msimu mmoja na kujiweka rekodi hiyo ndani ya ligi ya EPL nchini Uingereza wadau mbalimbali wameonyesha kukataa kuchukua kwa tuzo hiyo na kumpa nafasi Kelvin De Bruyne.

Mohamed Salah mwenye miaka 25 usiku wa jana aliweza kutangazwa kama mchezaji bora wa shirikisho akiwa amepambanishwa na wachezaji wengine wa EPL na kuwa mchezaji wa saba kutoka Liverpool kuchukua tuzo hiyo.

Hizi ni  takwimu za Mo Salah 

Mohamed Salah - Msimu wa 2017-18 

Ameshiriki mechi: 33
Mikwaju iliyogusa wavu: 64
Magoli: 31
Dakika alizocheza: 2,657
Amechangia magoli: 9
Nafasi alizotoa: 57
Mikwaju: 132
Pasi alizokamilisha: 684

Kwa upande wa De Bruyne mwenye miaka 26 ameweza kutoa mchango mkubwa akichangia magoli 15 na kutoa nafasi za kufunga magoli 104 ikiwa ni zaidi ya mchezaji mwingine katika msimu na kufanikiwa kufunga magoli 8.

Takwimu za De Bruyne.

Kevin de Bruyne - Msimu wa 2017-18 
 Ameshiriki mechi: 34
Mikwaju iliyogusa wavu: 36
Magoli: 8
Dakika alizocheza: 2,836
Amechangia magoli: 15
Nafasi alizotoa: 104
Mikwaju: 84

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...