Familia ya Alhaj Sudi Suleiman Madega, Katibu Mkuu (Mst) Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa Tanzania (TALGWU).

Inapenda kutoa shukrani zake za dhati kwa ndugu, jamaa na marafiki kwa msaada wa hali, mali na faraja walioipatia familia katika kipindi kigumu cha kuuguza, msiba na hatimaye kumpuzisha kwenye nyumba yake ya milele mpendwa wao Hajat Mwalimu Batoul Abdallah Mbarouk aliyefariki tarehe 16 Agosti, 2017 na kuzikwa tarehe 17 Agosti, 2017. 

Hajat Batoul A. Mbarouk alikuwa Mke wa Sudi S. Madega; na Mama wa Suleiman, Amir, Dr. issa, Maryam, Zuhura na Asha Madega. Pia, Mkwe wa Maryam Hamza Chum, Nuru Kassim Kisesa, Daud Buswelo na Hawa Kadyanji.

Kwa kuwa ni ngumu kumshukuru kila mmoja, itoshe kusema ahsanteni sana nyote. Hata hivyo, kipekee familia inapenda kufikisha salamu maalum kwa wafuatao:-
             i.        Madaktari, Wauguzi na Wafanyakazi wa Taasisi ya Saratani Ya Ocean Road ambako marehemu alikuwa akitibiwa tangu mwaka huu mwanzoni na hatimaye kuaga dunia tarehe 16 Agosti, 2017. Hususa, Dr. Steve, Dr. Kezia , Dr. Mathew, Dr. Chacha, Dr. Ruta  Dr. Abdi Sangali , Sister Sapine,  Sister Wema , Sister Ester , Sister Doris , Sister Kimath , Sister Eliza , Joel Makanyaga, Mkulia, Alawi, Solomon na wengine wote;
            ii.        Madaktari, Wauguzi na Wafanyakazi wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ambako marehemu alikuwa akitibiwa tangu mwezi Agosti, 2016;
           iii.        Mh. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais (Mst) wa Jamhuri Muungano wa Tanzania na mkewe Mh. Mwl. Salma Rashid Kikwete (Mb) na familia yao;
          iv.        Katibu Mkuu, Uongozi na Wafanyakazi wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa Tanzania (TALGWU);
            v.        Katibu Mkuu, Uongozi na Wafanyakazi wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT). Hususan, Makao Makuu, Mkoa wa Dar es Salaam, Mkoa wa Pwani na Walimu wote;
          vi.        Mh. Jaji (Mst) Harold R. Nsekela (Kamishna wa Maadili), Uongozi na wafanyakazi wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma;
         vii.        Mkurugenzi wa Uchaguzi Ndg. Kailima Ramadhani na Mkurugenzi wa Utawala Tume ya Taifa ya Uchaguzi Ndg. Hamis A. Mkunga;
        viii.        Alhaji Masoud Msangi, Mkurugenzi Mtendaji Nduvini Auto Works;
          ix.        Majirani wa marehemu wa Mbagala, Mbezi na Chang’ombe;
            x.        Vile vile, tunapenda kutambua familia zifuatazo:-
Ukoo wa Kanyama na Mbarouk popote pale walipo, Familia ya Mh. Luteni (Mst) Abdallah Kihato, familia ya Mh. Mohamed S. Jegame, familia ya Marehemu Balozi Isaya Bakari Chialo, familia ya Dr. Hamza Juma Chum, familia ya Brigedia Jenerali (Mst) Ussi Khamis wa Zanzibar, familia ya Kassim Kisesa, familia ya Masoud Sultan, familia ya Bakari O. Sangali, familia ya Issa Sechonge, familia ya Kisarazo, familia ya Idris Mavura, familia ya Marehemu Mwl. Hemed Ally Kimeah, familia ya Mbaruku Nguzo, familia ya Mbegu na wengine wote.

Pamoja na salamu hizi, familia inawaarifu na kuwaalika rasmi katika Arobaini ya Marehemu Mwalimu Mbarouk itakayofanyika nyumbani kwake Mbagala siku ya jumapili tarehe 24 Septemba, 2017 kuanzia saa 5 asubuhi mpaka 8 mchana.

Kwa mawasiliano tafadhali wasiliana na Ndg. Amir Sudi Madega kupitia Namba 0716875737.

Innalilahi Wainailahi Rajioun,
Ahsanteni Sana

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...