MSIMU wa tatu wa michuano ya BRAZUKA KIBENKI unaoshirikisha taasisi za kibenki katika michezo ya mpira wa miguu na kikapu unatarajiwa kuanza mwishoni mwa mwezi huu jijini Dar es Salaam.

Katika msimu huu michuano hiyo itashirikisha timu 15 ambazo ni NMB (Mabingwa watetezi), DTB, Barclay’s, BancABC, Exim, Stanbic, BOA, UBA, Letshego, EcoBank, CRDB, BOT, Azania, TPB, Access na UBA.

Mmoja wa maofisa wa benki ya Exim, Frank Rweyemamu ambaye pia ni mwanachama wa tawi la Simba Makini linalomiliki mtandao huu alivitaja viwanja vitakavyotumika kuwa ni Gymkhana na DonBosco.
Martin Komba wa DTB (kulia) akimtoka Hezbo wa NMB katika pambano la jana

“Michuano ya mwaka huu itafanyika katika viwanja vya Gymkhana kwa mpira wa miguu huku mechi za mpira wa kikapu zikitarajiwa kuchezwa katika uwanja wa DonBosco.” Alisema Rweyemamu.

Jana kulikuwa na mchezo wa ngao ya hisani ambapo mabingwa watetezi NMB walikubali kichapo cha mabao 4-0 kutoka kwa DTB katika mchezo wa kuashiria kuanza kwa michuano hiyo.

Bingwa wa msimu huu atakabidhiwa kikombe pamoja na medali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...